To advertise here, call: +255 655 611699

Kilimo cha miti ya matunda.


Upandaji miti ikiwemo Miti ya Matunda ni moja kati ya njia inayoweza kuwakwamua vijana kutokana na tatizo la ajira na umasikini. Ipo miembe iliyoboreshwa, miembe hiyo imetokana na kuunganishwa kwa miembe miwili tofauti. teknolojia ya ubebeshaji wa mimea inapelekea upatikanaji wa miembe yenye sifa ambazo wakulima wanazihitaji mfano ladha nzuri, ukubwa wa matunda na matunda yasiyo na nyuzinyuzi.

Miembe ya kubebeshwa huchukua muda mfupi kutoa mavuno kwani mwembe unaweza kutoa matunda ndani ya miaka miwili na nusu hadi mitatu tofauti na miembe ya asili ambayo huchukua muda si chini ya miaka mitano tangu kupandwa kuanza kutoa matunda. Na kwamba, embe la mwembe uliobebeshwa lililokomaa huwa linauwezo wa kuwa na kilo moja hadi kilo moja na nusu.

Share on Google Plus

About Funguka Tanzania

0 comments:

Post a Comment