Mwanamke akipenda anapenda kweli!
Mwanamke akikupenda anakuwa na furaha, anakuwa anajivunia kuwa na wewe, 
na hujihisi furaha kuongea na wewe.
Hupenda awe rafiki wa rafiki zako na ndugu zako, uvipendavyo na yeye 
atavipenda, atabadilisha mtindo wake wa maisha kuendana na mtindo wako.
Haitajalisha ni kiasi gani utamuudhi, atakusamehe hata kabla hujamuomba 
msamaha, atachokifanya ni kusubiri tu umuombe msamaha kuthibitisha kama 
kweli umejutia kosa lako.
Atajaribu kuwa na wivu na atakulinda kwani atahitaji uwe wake, wake peke
 yake na sio ku share. 
Atawakataa wengine wote wanaomtongoza kwa sababu 
ameona kesho yake ipo mikononi mwako.
Haitajalisha ni kiasi gani uko mbali na yeye, atajilinda kwa ajili yako.
 Atalike na ku comment kila kitu unachoweka facebook hata kama ni cha 
kipuuzi (hahaahaa).
Atakujibu kwa wakati text zako either watsapp, za kawaida au inbox ya 
fb. Hatajali kama unampa pesa au laa, kama ni tajiri au laa kwa sababu 
lengo lake ni kujenga maisha na wewe na sio kupass time ameona 
potentials kwako. 
 Atakuonyesha marafiki zake na ndugu zake, kwa sababu anajivunia kuwa 
mpenzi wako.
Tafadhali sana, muangalie mwanamke huyo, moyo wake umejawa na mapenzi, 
anastahili kutunzwa na kupendwa kama almasi.
Lakini tatizo kubwa la hawa "wavulana" (baadhi yao) baada ya kumfanya 
akupende zaidi, baada ya kupoteza muda wake juu yako, baada ya kuwakataa
 wanaume wengine ambapo kimsingi wengine walikuwa tayari kumuoa, baada 
ya kumuacha akutambulishe kwa ndugu zake na marafiki sasa unamuacha, 
unamkataa kwa mbwembwe nyingi, unamuacha akiwa na maumivu na aibu kubwa 
kwamba atawaambia nini wazazi wake, ndugu na marafiki, atatambulisha 
wangapi?
Na akiulizwa yuko wapi yule uliyetutambulisha? Awajibu nini!? Ofcoz 
atakachofanya ni kuinamisha kichwa huku ameshika mashavu! Hana jibu ni 
aibu na maumivu makubwa kwa kuwa alikupenda kwa dhati.
Mbona mnawaweka katika wakati mgumu wanawake waliopewa moyo wa kupenda? 
 Brothers, usimfanye mwanamke wako ajute kwanini alipenda, usifanye 
wengine wamcheke na kumdhihaki. Timiza ahadi yako, kama amekukosea na 
kukuomba msamaha jaribu kumpa nafasi ya pili. Kila mtu anahitaji nafasi 
ya pili ili aweze kurekebisha pale alipokosea.
Na nyie vijamaa mnaokua sasa, miaka 14 na kuendelea msiige tabia ya sisi
 kaka zenu, hiyo sio tabia njema kabisa. Jifunzeni kuheshimu hisia za 
mtu. Kujeruhiwa kihisia kunauma kuliko maumivu ya risasi.
Kama huna future nae usimtongoze na kumpa mimba.

0 comments:
Post a Comment