Vyakula vya kuku vinaweza kupatikana madukani au kutengenezwa na mfugaji
mwenyewe. Ili kuku aweze kukua haraka na kutoa mazao mengi na bora ni lazima
chakula kitengenezwe katika mchanganyiko wenye uwiano mzuri uliopendekezwa.
Chakula hicho lazima kiwe na viinilishe muhimu kama vile protini, wanga, madini
na vitamini. Hakikisha chakula unachotengeneza kina mchanganyiko wa vyakula
vifuatavyo:
i.
Vyakula vya kujenga mwili kama vile jamii ya kunde, samaki, dagaa,
mashudu ya ufuta, pamba na alizeti.
ii.
Vyakula vya kulinda na kukinga mwili usipate maradhi kama vile mafuta ya
samaki na majani mabichi kama kabichi, michicha, majani ya mpapai na nyasi
mbichi.
iii.
Vyakula vinavyojenga mifupa kama vile aina ya madini, chokaa, mifupa
iliyosagwa na chumvi. Ukosefu wa vitamini na madini kama Kalsiamu na Fosforasi
husababisha matege, kukunjamana kwa vidole, kufyatuka kwa misuli ya goti na
kupofuka macho.
Maji ni muhimu sana kwani husaidia kulainisha na kurahisisha usagaji wa
chakula, na kupunguzajoto. Wakati wajoto kali kuku wapewe maji mengi.
Kabla ya Kutengeneza Chakula Lazima Mtengenezaji
Ajue haya Yafuatayo:-
i.
Jinsi ya kupata vyakula vya aina mbali mbali.
ii.
Kiasi cha viinilishe vinavyohitajika kwa kuzingatia umri na aina tofauti
ya kuku; kwa mfano vifaranga wanahitaji protini asilimia 18 hadi 22, kuku
wanaokua asilimia 17 hadi 19 na kuku wa mayai asimilia 15 hadi 17. Vile vile
madini aina ya Kalsiamu kiasi cha asilimia tatu hadi nne kinahitajika kwa kuku
wa mayai na asilimia moja kwa kuku wa nyama na vifaranga.
iii.
Viwango vya uchanganyaji wa aina za vyakula mbali mbali: Ili
mtengenezaji aweze kutengeneza chakula bora ni muhimu afuate kiwango cha
uchanganyaji kilichopendekezwa Kiasi cha aina moja ya chakula kinapozidi
kinaweza kuleta madhara.
Jedwali lifuatalo linaonyesha kiwango kinachotakiwa kwa baadhi ya
vyakula.
Vyakula na Viwango Vinavyohitajika katika Asilimia
100
Aina ya Chakula
|
Kiwango cha
Uchanganyaji (%)
|
||
Vyakula
|
Vifaranga
|
Kuku wa Nyama
|
Kuku wa Mayai
|
Mahindi
|
70
|
70
|
70
|
Ulezi
|
20
|
40
|
40
|
Mtama
|
20
|
30
|
30
|
Mpunga
|
40
|
70
|
70
|
Ngano
|
5
|
40
|
40
|
Pumba za mahindi
|
10
|
20
|
20
|
Pumba za Mpunga
|
10
|
20
|
20
|
Pumba za Mtama
|
10
|
20
|
20
|
Pumba za Ngano
|
5
|
15
|
15
|
Mashudu ya nazi
|
10
|
30
|
40
|
Mashudu ya Pamba
|
5
|
10
|
5
|
Mashudu ya Alizeti
|
10
|
20
|
20
|
Mashudu ya Ufuta
|
10
|
10
|
5
|
Damu iliyokaushvva
|
5
|
5
|
5
|
Mifupa iliyosagwa
|
5
|
5
|
7.5
|
Dagaa
|
10
|
5
|
5
|
Lusina iliyosagwa
|
|||
(Lucerne meal) Lukina
|
5
|
5
|
5
|
(Lcuecana meal)
|
2.5
|
5
|
5
|
Chokaa
|
5
|
5
|
5
|
Chumvi
|
0.5
|
0.5
|
0.5
|
Soya
|
10
|
20
|
20
|
Kuhusu kiasi cha viinilishe kama protini, wanga, madini na
vitamini vilivyomo kwenye aina za vyakula vitakavyochanganywa, Mfugaji
anashauriwa amuone mtaalamu wa mifugo aliyekaribu naye aweze kumsaidia na kumpa
ushauri zaidi.·
Mchanganyiko uwe na zaidi ya aina moja ya vyakula kwa mfano
vyakula vya kujenga mwili vitokanavyo na wanyama na mimea.·
Mifano ya kutengeneza kilo 100 za chakula cha
kuku:-
Mfano wa chakula cha vifaranga kuanzia siku
ya kwanza hadi majuma manne.·
Vyakula
|
Kiasi (Kg)
|
Mahindi
|
30.00
|
Pumba za Mahindi
|
20.00
|
Soya
|
18.00
|
Mashudu ya Alizeti
|
20.50
|
Dagaa
|
5.00
|
Mifupa iliyosagwa
|
4.00
|
Chumvi
|
0.50
|
Vitamini
|
2.00
|
Jumla
|
100.00
|
Mfano wa chakula cha kukuzia kuanzia Juma la
nne hadi la nane.·
Vyakula
|
Kiasi (kg)
|
Mahindi
|
45.00
|
Pumba za Mahindi
|
20.00
|
Mashudu ya pamba
|
5.00
|
Soya
|
20.00
|
Dagaa
|
2.50
|
Mifupa iliyosagwa
|
5.00
|
Chumvi
|
0.50
|
Vitamini
|
2.00
|
Jumla
|
100.00
|
Mfano wa chahula cha kuku wa mayai kuanzia
Juma la nane hndi la ishirini.·
(a)
|
(b)
|
||
Vyakula
|
Kiasi (Kg)
|
Vyakula
|
Kiasi (Kg)
|
Mahindi
|
45.00
|
Mahindi
|
45.00
|
Pumba za mahindi
|
25.00
|
Pumba za mahindi
|
30.00
|
Soya
|
5.00
|
Soya
|
5.00
|
MashuduyaAlizeti
|
10.00
|
Mashudu ya pamba
|
5.00
|
Dagaa
|
4.00
|
Dagaa iliyokaushwa
|
4.00
|
Damu
|
3.00
|
Mifupa iliyosagwa
|
2.50
|
Chokaa
|
3.00
|
Chokaa
|
3.00
|
Chumvi
|
0.50
|
Chumvi
|
0.50
|
Vitamini
|
2.00
|
Vitamini
|
2.00
|
Jumla
|
100.00
|
100.00
|
Mfano chakula cha kuku wa Mayai kuanzia Juma
la lshirini na kuendelea:·
(a)
|
(b)
|
||
Vvakula
|
Kiasi (Kg)
|
Vvakula
|
Kiasi (kg)
|
Mahindi
|
50.00
|
Mahindi
|
40.00
|
Pumba za mahindi
|
15.00
|
Pumba za mahindi
|
25.00
|
Mashudu ya Pamba
|
5.00
|
Mtama
|
5.00
|
Soya
|
18.00
|
Mashudu ya Alizeti
|
10.00
|
Dagaa
|
4.50
|
Dagaa
|
4.00
|
Mifupa iliyosagwa
|
3.00
|
Damu ilyosagwa
|
5.00
|
Chokaa
|
2.00
|
Mifupa iliyosagwa
|
4.50
|
Chumvi
|
0.50
|
Chokaa
|
4.00
|
Vitamini
|
2.00
|
Chumvi
|
0.50
|
Jumla
|
100.00
|
Vitamini
|
2.00
|
Jumla
|
100.00
|
0 comments:
Post a Comment